Haki za watoto na vijana

Lærerinnhold

Tips til undervisningen

Det at det finnes en barnelov i Norge, er et eksempel på en av kjerneverdiene i samfunnet: Alle mennesker er likeverdige og beskyttet av lover og rettssystemet, uavhengig av legning, funksjonsevne, seksualitet og alder. Barn har det samme rettsvernet som voksne.

Tips til undervisninga

Det at det finst ei barnelov i Noreg, er eit døme på ein av kjerneverdiane i samfunnet, nemleg at alle menneske er likeverdige og er verna av lover og rettssystemet, uavhengig av legning, funksjonsevne, seksualitet og alder. Barn har det same rettsvernet som vaksne.

Læreplan

Grunnleggende ferdigheter

Digitale ferdigheter
Muntlige ferdigheter

Tverrfaglige tema

Folkehelse og livsmestring

Læreplan i samfunnskunnskap for voksne innvandrere etter integreringsloven

gi eksempler på viktige lover, regler og verdier som omhandler barn og unges rettigheter og rettsvern

Kjerneelement

Individ og fellesskap

Læringsaktivitet

Muntlig aktivitet

Haki za watoto na vijana

En jente i toårsalderen står i en eng. Hun holder en løvetann og smiler bredt. Foto
GettyImages

Haki za watoto na vijana

Tuna sheria nchini Norwe inayojulikana kama Sheria ya watoto. Inatumika kwa watoto na vijana walio chini ya umri wa miaka 18 na inabainisha majukumu ya wazazi kwa watoto wao pamoja na haki za watoto

Hapa kuna maelezo muhimu kuhusu Sheria ya watoto:

  • Mtoto anapozaliwa, ofisi ya Sajili ya Kitaifa ya Watu inaarifiwa. Notisi sharti ieleze mama na baba ni nani na ikiwa wanaishi pamoja.
  • Kimsingi, wazazi wana jukumu kuu kwa watoto wao, na watoto wana haki ya kutunzwa na kushughulikiwa na wazazi wao.
  • Wazazi wanapaswa kuhakikisha kuwa mtoto anapata chakula na mavazi na vitu vingine anavyohitaji ili kuwa na maisha mazuri hadi atakapofikisha miaka 18.
  • Wazazi wana jukumu la kuwapa watoto wao malezi mazuri, na lazima kila wakati wazingatie maslahi na mahitaji ya watoto wao. Sheria ya Watoto inapiga marufuku vurugu katika kuwalea watoto.
  • Wazazi sharti wahakikishe watoto wao wanahudhuria masomo ya lazima ya shule ya msingi na sekondari na kuwa wanapata elimu inayolingana na uwezo na masilahi yao.
  • Watoto wana haki ya kuwaona wazazi wao wote, ikijumuisha ikiwa hawaishi pamoja.
  • Wazazi wana jukumu na haki ya kuwafanyia maamuzi watoto wao wakati watoto hawawezi kujiamulia wenyewe. Wazazi wanapaswa kuzingatia zaidi maoni ya mtoto kadri anavyoendelea kukua. Watoto waliofikisha umri wa miaka saba wana haki ya kutoa maoni yao kabla ya wazazi kufanya maamuzi kuhusu masuala ya kibinafsi yanayomhusu mtoto. Sheria hii inasema kuwa mtoto anapofikisha miaka 12, maoni yake ni ya umuhimu mkubwa.
  • Watoto ambao wamefikisha miaka 15 wana haki ya kufanya maamuzi katika masuala yanayohusiana na elimu na kujiunga au kuondoka kwenye mashirika.
  • Umri wa kuwa mtu mzima nchini Norwe ni miaka 18. Hii inamaanisha kuwa mtoto amefikisha umri ambapo anaweza kuingia katika mikataba ya kisheria na kuwa na udhibiti wa pesa zake mwenyewe. Wazazi hawawajibikii mtoto tena.

Jadilianeni pamoja

Jente tenker  på hva slags klær hun vil velge. Foto
Ninataka sweta nyekundu!
Far og sønn forbereder seg til fotballtrening. Foto
GettyImages Sitaki kwenda kufanya mazoezi ya soka tena.
Sønn snakker med mot. Foto
Ninataka kuwasilisha ombi la kufanya kozi ya ujenzi kwenye shule ya sekondari.
Mor snakker til sønn. Foto
GettyImages Je, hungependa kufanya kazi ya kuvutia zaidi? Unapenda hisabati. Unaweza kusomea uhandisi.
  • Zungumzia kuhusu picha. Je, zinahusiana vipi na Sheria ya watoto?
  • Je, kuna sheria maalum inayowalinda watoto katika nchi zingine unazojua?
  • Je, Sheria ya watoto inamaanisha nini kwa wazazi?
  • Je, mtoto anahitaji nini ili kuwa na maisha mazuri?
  • Je, wazazi wana jukumu gani katika mtoto wao wa umri wa miaka 15 anapochagua elimu ya sekondari?
  • Je, kifungu gani katika Sheria ya watoto unachukulia kuwa muhimu zaidi?

Chagua jibu sahihi

Je, Sheria ya watoto inahusu nani?

Chagua jibu sahihi

Je, Sheria ya watoto inasema nini kuhusu vurugu katika kuwalea watoto?

Chagua jibu sahihi

Je, ni nani anayewajibika kuhakikisha kuwa watoto wanapata elimu ya shule ya msingi?

Chagua taarifa sahihi au isiyo sahihi

Soma taarifa hizi. Ipi ni sahihi? Ipi si sahihi?

Sheria ya watoto inasema mengi kuhusu majukumu ya wazazi kwa watoto.
Watoto ambao wamefikisha umri wa miaka 15 wanaweza kujiamulia wenyewe ikiwa wangependa kujiunga au kuondoka kwenye mashirika ya kidini na ya kisiasa.
Ikiwa wazazi hawaishi pamoja, mtoto anaruhusiwa tu kumwona mama.
Umri wa kuwa mtu mzima nchini Norwe ni miaka 16.
Mtu anapofikisha miaka 18, sio wazazi tena wana jukumu la kisheria na kifedha.

Chagua taarifa sahihi au isiyo sahihi

Soma taarifa hizi. Ipi ni sahihi? Ipi si sahihi?

Mtoto anapozaliwa, ofisi ya Sajili ya Kitaifa ya Watu inaarifiwa.
Watoto wana haki ya kutunzwa na wazazi wao.
Wazazi sharti wahakikishe kuwa watoto wao wanapokea chakula na mavazi hadi watakapofikisha umri wa miaka 15.
Wazazi wana jukumu na haki ya kuwafanyia maamuzi watoto wao wakati watoto hawawezi kujiamulia wenyewe.