kuchambua mambo kwa makini na kuelewa maadili

Lærerinnhold

Tips til undervisningen

Snakk sammen

Det er viktig å snakke sammen om hvordan man kan vurdere hvor troverdig informasjon er. Vi blir alle bombardert med informasjon fra ulike kilder. Noen ganger får vi motstridende informasjon. Hvem skal man da stole på? Har avsender av informasjon en egen agenda? Skal man for eksempel stole på informasjon fra myndighetene eller fra venner om informasjonen er motstridende?

Hvordan blir det hvis barna lærer ikke å si i mot foreldrene hjemme og samtidig lærer i barnehagen eller på skolen å stille spørsmål og argumentere?

Tips til undervisninga

Snakk saman

Det er viktig å snakke saman om korleis ein kan vurdere kor truverdig informasjon er. Vi blir alle bombarderte med informasjon frå ulike kjelder. Nokre gonger får vi motstridande informasjon. Kven skal ein då lite på? Har avsendaren av informasjonen ein eigen agenda? Skal ein til dømes lite på informasjon frå styresmaktene eller frå vener dersom dei gjev motstridande informasjon?

Korleis blir det dersom barna heime lærer å ikkje seie imot foreldra og samstundes lærer i barnehagen eller på skulen å stille spørsmål og argumentere?

Læreplan

Grunnleggende ferdigheter

Digitale ferdigheter
Muntlige ferdigheter

Tverrfaglige tema

Demokrati og medborgerskap

Læreplan i samfunnskunnskap for voksne innvandrere etter integreringsloven

bruke kunnskap om personvern og opphavsrett, samt retten en selv og andre har til privatliv
samtale om betydningen av kritisk tenkning og etisk bevissthet, blant annet knyttet til digital dømmekraft

Kjerneelement

Perspektivmangfold og kritisk tenkning

Læringsaktivitet

Muntlig aktivitet

kuchambua mambo kwa makini na kuelewa maadili

Seks personer står ved siden av hverandre. De holder opp tankebobler og snakkebobler laget med papir i forskjellige farger. Bildet illustrerer at de har forskjellige meninger. Foto
GettyImages

Leo, kuna msisitizo nchini Norwe kuwa kila mtu aruhusiwe kutoa maoni yake. Watoto hujifunza shuleni kuwa na hamu ya kufahamu mambo na kutumia maarifa wanayopata ili kufanya maamuzi yanayofaa. Wanajifunza kuwazia mambo, kujadili na kuwa wabunifu. Haitoshi tu kurudia alichosema mwalimu au kilichoandikwa kwenye vitabu. Ili kukuza maarifa na ufahamu mpya, sharti uulize maswali na utathmini mambo yayochukuliwa kuwa ya kweli. Pia, lazima ufahamu kuwa kuna uwezekano kwamba huenda ujuzi na uzoefu wako una upungufu fulani.

Et nærbilde av et forstørrelsesglass foran en PC-skjerm. Bildet illustrerer at man bør granske kildene sine. Foto
GettyImages

Tunaishi katika jamii ambapo maelezo yanapatikana kote. Hakuna mtu anayeweza kuhifadhi habari yote akilini. Hii inamaanisha kwamba ni muhimu kujua mahali habari inakopatikana na jinsi ya kuifikia. Miongoni mwa mambo mengine, lazima tujifunze kutumia Intaneti na kutafuta habari kwenye vitabu. Mtu yeyote anaweza kuchapisha maelezo mtandaoni, na sio habari zote zinazopatikana hapo ni sahihi. Ndio maana tunapaswa kuchambua vyanzo.

Kuchambua vyanzo inamaanisha kutathmini unachosoma. Msomaji lazima ajiulize maswali muhimu, k.m.:

  • Je, aliyeandika ni nani?
  • Je, aliyeandika ana nia mahususi?
  • Je, madhumuni yake ya kuandika makala haya ni gani?
  • Je, maelezo ni sahihi?
  • Je, maelezo yote muhimu yamejumuishwa, au yapo maelezo yaliyoachwa nje?

Ikiwa tutatumia maandishi ya watu wengine, picha, muziki, nk. katika matoleo yetu wenyewe, lazima kila wakati tueleze ni nani ana hakimiliki ya vipengee hivyo.

Uelewa wa maadili unahusu kuangalia vigezo mbalimbali, ili uone chaguo zako na ufanye uamuzi bora. Hii itakuwezesha kufanya kile kinachofaa kwa jamii, watu walio karibu nawe na kwako mwenyewe.

  • Uelewa wa maadili, unaomaanisha kuangalia vigezo mbalimbali, ni muhimu katika kukuwezesha kuwa mtu wa kuwazia mambo na mwenye kuwajibika. Masomo na mafunzo sharti yakuze uwezo wa wanafunzi wa kufanya tathmini za kimaadili na kumsaidia kutambua masuala ya maadili.
  • Kuchambua mambo kwa makini na kuelewa maadili kunahitajika na ni sehemu ya kile kinachochukuliwa kuwa kujifunza katika hali anuwai na hivyo itawasaidia wanafunzi kuweza kufanya maamuzi yanayofaa.

Chanzo: Idara ya Elimu

Jadilianeni pamoja

  • Je, kuchambua chanzo ni nini?
  • Je, kuna umuhimu gani kwa wanafunzi na watu wengine kuuliza maswali kuhusu wanachosoma mtandaoni?
  • Shule nchini Norwe zinahimiza wanafunzi kufikiria na kuwa na mitazamo yao binafsi. Je, unachukulia hili vipi? Je, kwa nini iko hivyo? Je, inaathiri malezi ya watoto na uhusiano kati ya watoto na wazazi wao?

Familia ya watu wanne inahitaji gari mpya. Gari litatumika kwa safari ndefu na fupi. Martin na Maria hawajui cha kuchagua.
1. Gari kubwa lenye viti sita wanaloweza kutumia kwa safari ndefu na fupi. Gari lina nafasi ya kubebea nyanya na babu, na linatumia dizeli.
2. Gari la umeme lenye viti vinne linalofaa kwa safari fupi za familia, lakini linahitaji chaji njiani wakati wa safari ndefu za familia, na halina nafasi ya kubebea babu na nyanya.

Martin na Maria hawangependa kuathiri mazingira, na wao ndio jamaa wa karibu wa babu na nyanya. Je, unadhani Martin na Maria watajadili masuala yepi ya kimaadili?

Mann og kvinne sitter med en pc og diskuterer. Foto
GettyImages

Chagua jibu sahihi

Je, kuchambua chanzo ni nini?

Chagua jibu sahihi

Je, ni hali ipi itafaa nchini Norwe?

Chagua jibu sahihi

Je, unapaswa kuchunguza nini unaposoma kitu fulani kwenye mtandao? Unaweza kuchagua zaidi ya jibu moja.

Chagua taarifa sahihi au isiyo sahihi

Soma taarifa hizi. Ipi ni sahihi? Ipi si sahihi?

Maelezo yanayopatikana mtandaoni ni sahihi.
Nchini Norwe, lengo ni kukubali.
Uelewa wa maadili unahusu kuangalia vigezo mbalimbali ili uone chaguo zako na ufanye uamuzi bora.
Kuchambua chanzo ni kutokubaliana na unachosoma.
Kuchambua mambo kwa makini na kuelewa maadili humwezesha mtu kufanya maamuzi bora.

Chagua taarifa sahihi au isiyo sahihi

Soma taarifa hizi. Ipi ni sahihi? Ipi si sahihi?

Unaposoma maelezo mtandaoni, unapaswa kujiuliza maswali muhimu.
Shuleni, watoto hujifunza kuwa na mitazamo tofauti.
Wakati mwingi, kuchambua mambo kwa makini na kuelewa maadili kunahitajika na ni sehemu ya kujifunza.
Watu walioidhinishwa pekee ndio wanaweza kuchapisha maelezo mtandaoni.
Ili maarifa na ufahamu mpya ukuzwe, sharti mtu aulize maswali na atathmini mambo yanayochukuliwa kuwa ya kweli.